MAKAMISHINA BUNGE LA NIGERIA WATEMBELEA DARAJA LA KIGAMBONI, DAR ES SALAAM TANZANIA

Hili ndio Daraja la kisasa la Kigamboni, lililoko eneo la Kurasini, Manispaa ya Temeke, Jijini Dar es Salaam. Daraja ambalo wahandisi wanasema litazinduliwa rasmi na Rais Jakaya Kikwete, Oktoba Mwaka huu kabla ya hajastaafu nafasi hiyo.

Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kigamboni kutoka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mhandisi Karim Mataka (kushoto), akionyesha sehemu ya mradi wa daraja hilo kwa Makamishna kutoka Bunge la Nigeria, Bi. Barr Lamnye (kulia), Alhaj Aliyu Abubakar (wa pili kulia) na Kiongozi wa msafara huo Bw. Elder Stephen Yepwi, walioko nchi kwa ziara ya kikazi.



Mhandisi Karim Mataka kutoka NSSF (wa pili kulia), akiwaelekeza jambo Makamishna wa Bunge la Nigeria, Bw. Elder Stephen Yepwi (wa tatu kushoto) na Alhaj Aliyu Abubakar (wa pili kushoto), walipotembelea ujenzi wa daraja hilo, Dar es Salaam leo. Kulia ni Mhandisi Mohamed Abdepbay na Mhandisi Liu Too (kushoto).

Kiongozi wa msafara wa Makamishna wa Bunge la Nigeria, Bw. Elder Stephen Yepwi (wa pili kulia), akifafanua jambo kwa Meneja Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kigamboni, kutoka shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mhandisi Karim Mataka (wa pili kushoto), baada ya Makamishna wa Bunge la Nigeria kutembelea daraja hilo, Dar es Salaam leo.
 Wakijadiliana jambo baada ya Wabunge hao kuvutiwa na mradi huo mkubwa.



Hili ndio Daraja la kisasa la Kigamboni.
 

Hii ni Barabara Kuu inazotoka kwenye Daraja la Kigamboni, kwa ajili ya kuungana na barabara Kuu ya Mandela, ikiwa katika hatua ya mwisho

Hii ni sehemu ya Daraja la Kigamboni ambayo ujenzi wake umekamilika.



Kipande cha Daraja la Kigamboni kinachosubiri kuuganishwa na njia kuu.



Meneja Mradi wa ujenzi wa Daraja la Kigamboni kutoka Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mhandisi Karim Mataka akizungumza na Makamishna hao baada ya kutembelea mradi huo, Dar es Salaam leo.

Comments

HABARI ZILIZOPITA

HEKAYA ZA ABUNUWASI

HISTORIA YA VITA VYA KAGERA 1978 - 79

PATA HADITHI ZA UPELELEZI ZA KUSISIMUA

TUTARUDI NA ROHO ZETU?

Vifaa vya Kijeshi vilivyotia fora maonesho ya miaka 50 ya Uhuru

HOFU